Tetemeko la Ardhi nchini Peru
Tarehe 18 Julai, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 3.7 liliupiga mkoa wa JunÃn, karibu na wilaya ya vijijini ya Chongos Bajos nchini Peru. Ripoti za awali zilionyesha kwamba takribani nyumba 48 zilikuwa zimeteketezwa na nyingine 18 zilikuwa zimeharibiwa, hivyo kuathiri takribani watu 300.Airbnb.org inashirikiana na TECHO Internacional ili kutoa makazi ya dharura bila malipo kwa wafanyakazi muhimu.
Ikiwa ungependa kusaidia kutoa sehemu za kukaa bila malipo kwa watu walioathiriwa na tetemeko la ardhi, unaweza kutoa mchango kwenye Airbnb.org. Asilimia 100 ya michango huenda moja kwa moja kwenye makazi ya dharura. Ikiwa wewe ni mwenyeji wa Airbnb, unaweza kujisajili ili kutoa ukaaji wenye punguzo kwa wakazi walioathiriwa. Airbnb hutoa ada zake za huduma za mwenyeji kwa Airbnb.org kwa ajili ya sehemu hizi za kukaa na huwapa wenyeji AirCover kwa kila nafasi inayowekwa.