Mlipuko wa bomba la gesi nchini Malesia

Majirani wakiwasaidia majirani

Wanatimu watatu wa HostPlatform nchini Malesia wamesimama pamoja

Jayden aliposikia kuhusu bomba la gesi ambalo lililipuka huko Putra Heights mwezi Aprili mwaka 2025, mara moja aliwasiliana na mtandao wake ili kusaidia watu ambao walikuwa wamehamishwa makwao na maafa hayo.Kama Mkurugenzi Mtendaji wa HostPlatform, Jayden anafanya kazi na maelfu ya wenyeji kote nchini Malesia na Kusini-Mashariki mwa Asia ili kuwasaidia kusimamia matangazo yao. Kwa hivyo, alipogundua kuwa Airbnb.org ilikuwa ikitoa makazi ya dharura ya wiki mbili bila malipo kwa watu walioathiriwa na mlipuko, yeye na wenzake, Ken na Eunice, waliwahimiza wenyeji huko Putra Heights kufanya nyumba zao zipatikane kwa wale walio na uhitaji.

Watu watatu kutoka timu ya HostPlatform wamesimama kwenye uwanja wakitazama jiji

“Tunajivunia kuweza kusaidia na kuiauni jumuiya kwa sababu hili ni jukumu letu kama Wamalesia”

Kujizatiti kwao kulienea zaidi ya kutoa msaada, walihudhuria pia mikutano ya jumuiya kwenye makao ambapo manusura wengi walikuwa wakikaa, wakiwasaidia kujisajili kupitia Airbnb.org

Jihusishe

Jiunge na jumuiya ya kimataifa inayotoa makazi ya dharura wakati wa shida.

Pata maelezo zaidi

Kila sehemu ya kukaa ina simulizi

Kutana na watu walioathiriwa na majanga na wale waliosaidia.